Posts

Showing posts from March, 2023

MELI KUBWA ZA MIZIGO ZAENDELEA KUTIA NANGA BANDARI YA TANGA

Image
Meli ya mizigo yenye  urefu wa mita 179 ambayo imekuja na magari kutoka china China  ikiwa ni mara ya kwanza kushushwa magari bandarini hapo baada ya maboresho ya ujenzi wa gati lenye urefu wa mita 450. Meneja wa bandari ya Tanga Masoud Mrisha akitoa maelezo kwa mkuu wa mkoa wa Tanga Wazitri Kindamba mara baada ya kufanya ziara yake ya siku moja kutembelea bandarini hapo march 15,2023. Mkuu wa mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungumza mara baada ya kutembelea bandari ya Tanga kushoto kwake ni meneja wa bandari hiyo Masoud Mrisha. Na Denis Chambi,  Tanga. Matokeo chanya ya maboresho yaliyofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais  Dkt. Samia Suluhu Hassan  katika bandari ya Tanga yanaendelea kuonekana kufwatia meli kubwa za mizigo kutoka nje ya nchi  zikiendelea kutia nanga wafanyabiashara wakizidi kuitumia hatua ambayo inakwenda kuongeza biashara shindani katika ukanda wa Afrika mashariki. Ukiachana na meli kubwa iliyopokelewa hivi karibuni...

Fainali ya FA kupigwa Uwanja wa Mkwakwani.

Image
          Meneja wa uwanja wa CCM  Mkwakwani Nassoro Makau 'Nassa' akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na maandalizi ya fainali ya mchezo wa kombe Shirikisho la Azam utakaochezwa katika dimba hilo.   Na Denis Chambi,  Tanga. Mkoa wa Tanga umepokea kwa furaha kubwa taarifa za  kutangazwa kuwa mchezo wa fainali  ya kombe la Shirikisho la Azam   utachezwa katika dimba la CCM Mkwakwani kwa  msimu huu wa 2022/2023. Meneja wa uwanja CCM Mkwakwani Nassoro Makau 'Nassa' alisema wamepokea kwa bashasha taarifa hizo kuona kwamba uwanja wao unakidhi vigezo vya  kuchezwa fainali hizo huku akiahidi kwenda kuyafanyia marekebisho baadhi ya maeneo ambayo bado hayajakaa sawa kulingana na hadhi ya mashindano hayo. "Hii ni fursa kubwa sana ambapo tunategemea kupata mashabiki wengi kutoka wilaya za mkoa wetu na kutoka  mikoa mingine  tofauti tofauti kuja kuangalia fainali hii katika mkoa wetu wa Tanga kwetu...